Huenda utofauti wa tamaduni na mazoea ya watu inafanya
baadhi ya vitu pia kutofautiana.. zipo story za watu kula mbwa na wanyama
wengine, huku kwetu sio kawaida.
Kumbe China kuna soko la nyama ya punda? Kuna maeneo
ukienda utakuta punda wanatumiwa kubebea mizigo basi, lakini kwa China punda ni
nyama yenye soko kubwa tu.
Eneo la Maraigishu mji wa Naivasha, Kenya
kuna story ya ujenzi wa eneo la kiwanda cha machinjio ya punda kuelekea
kukamilika, ambapo tayari nyama hiyo ina soko la uhakika ndani ya
China.
Msimazi wa ujenzi huo Stephen
Kairuki amesema ujenzi huo umekamilika kwa 80%, eneo hilo litakuwa
na Ofisi za kiwanda hicho pamoja na maabara maalum ya kupima nyama kabla ya
kupakiwa, pia kutakuwa na mashine maalum ya kuchinjia punda na kuwachuna
ngozi.
Fundi huyo amepata nafasi ya kufanya mahojiano na
ripota wa CHENGULA NEWZ ambapo
amesema wanakijiji wa eneo hilo watapewa punda wawili wa kufuga; “sio
kila mtu bali wakulima wa eneo hili watapewa punda wa kike na wakiume, wakulima
wanatarajiwa kuwafuga na kuwauzia kiwanda hicho kila
wanapokomaa“
Kutokana na mahitaji ya soko la nyama hiyo China, kwa
siku watatakiwa kuchinjwa punda 70, mbali na uhitaji wa nyama pia kuna
wafanyabiashara waliotoka Marekani ili kuingia makubaliano ya kununua ngozi ya
mnyama huyo kwa ajili ya kutengenezea dawa ya vipodozi vya
wanawake.
Kingine kitakachowanufaisha wanakijiji kutoka kwenye
kiwanda hicho ni huduma ambazo watasogezewa kutokana na mradi huo kuwa kwenye
kijiji hicho ikiwemo huduma ya maji, hospitali na ajira kwa zaidi ya vijana
100.
Ufunguzi wa mradi huo utafunguliwa ndani ya kipindi cha
miezi miwili kuanzia sasa.
No comments:
Post a Comment