Tuesday 28 April 2015

BARCELONA YA IMALIZA GETAFE

1430247736623_lc_galleryImage_Barcelona_s_Luis_Suarez_f
CAMP Nou ni sehemu ya machinjio! hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada ya Barcelona kuichapa Getafe magoli 6-0 katika mechi ya ligi kuu Hispania, La Liga iliyomalizika usiku huu.
Mapema dakika ya 9′ Lionel Messi aliandika goli la kuongoza kwa mkwaju wa penalti na katika dakika ya 25′ Luis Suarez alipiga bao la pili.
Dakika ya 28′ Neymar Jr akapiga goli la tatu na chuma cha nne kimetiwa kambani na Xaiv Hernandez.
Suarez alitikisa tena nyavu dakika ya 40′ akifunga goli la tano na Messi akamaliza shughuli dakika ya 47′ akifunga goli la sita

No comments:

Post a Comment