Saturday 9 May 2015

DADA AJUTIA NDOA

Na Paul Chengula 



   MWANAMKE  ajulikanae kwa jina la mwasiti juma ,mkazi wa songea ameelezea matatizo yalio mkuta siku alipo unguzwa na mumewe ajulikanae kwa jina la muhammed ally mkazi wa songea vijijini,kisa pombe

mwanamke huyo ambae amekutwa na mkasa huo ambapo alipokutwa na mumewe nyakati za usiku wakati yeye akihudumia nguruwe kwa kutoa uchafu kwenye boma la nguruwe

   ndipo alipoingia mume wake na kumtaka aache kazi alizokuwa akizifanya na kumfata jikoni ambapo   mwasiti alikuwa amembandikia mumewe maji ya kuoga ,mume huyo ndipo alipo anza kumshutumu mama huyo kwa kosa la kuchelewa kupika mpaka muda anao fika yeye kwanini hajamaliza kupika

  Pia baada ya kumsema mwasiti ndipo baba huyo alipo amua kuchukuwa sefuria la maji lililo kuwa jikoni na kumwagia mama huyo ambae  alikuwa amejifunga kitenge

  Mashuhuda wa tukio hilo walipo zungumza na  CHENGULA NEWZ walisema kuwa baba huyo amekuwa akimtukana mwasiti kila anapo kuwa akirudi nyumbani ambapo maranyingi huwa anarudi akiwa amelewa ,pia majirani waliiambaia CHENGULA NEWZ kuwa baba huyo ni balozi wa nyumba kumi katika kijiji chao hivyo mwasiti  amekuwa akipigwa na kukosa sehemu ya kupeleka matatizo yake.

No comments:

Post a Comment