CHENGULA     NEWS

CHENGULA NEWS

CHENGULA NEWS

  • NYUMBANI
  • MICHEZO
  • BURUDANI
  • HABARI
  • MATUKIO
  • chengula news.com
  • UCHUMI

Saturday, 9 May 2015

MSUVA AULA AFRICA KUSINI

  MFUNGAJI bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Simon Msuva anarejea jioni ya leo Dar es Salaam na tabasamu ‘kuubwa’ baada ya kufaulu majaribio ya kucheza soka ya kulipwa Afrika Kusini.
Winga huyo wa mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga SC jana amekamilisha majaribio yake ya siku tatu Bidvest Wits ya Ligi Kuu nchini humo na matokeo ni ‘safi’.
  CHENGULA NEWZ inafahamu Bidvest Wits wameridhika na uwezo Msuva na sasa wanafungua majadiliano na klabu yake, Yanga SC.
Msuva amebakiza mwaka mmoja katika Mkataba wake Yanga SC na Wits iko tayari kutumia si zaidi ya dola za Kimarekani 100,000 (Sh. Milioni 200) kukamilisha dili zima la mchezaji huyo- kwa maana ya malipo ya mchezaji kusaini na ada ya uhamisho kwa klabu yake.  
Msuva aliondoka Dar es Salaam Jumatano wiki hii akiwa tayari ameipa Yanga SC ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, huku pia akiwa anaongoza kwa mabao, 17 akifuatiwa na mchezaji mwenzake wa timu hiyo, Amissi Tambwe mabao 14.   Amekosa mechi mbili za mwisho dhidi ya Azam FC Yanga ikilala 2-1 na leo dhidi ya Ndanda ya Mtwara.
Tangu ajiunge na Yanga SC mwaka 2012 akitokea Moro United, Msuva ameifungia timu hiyo mabao 35 jumla katika mechi 102 za mashindano yote
Posted by Unknown at 05:41
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

TANGAZO

TANGAZO
SOMA CHENGULA NEWS

KUNIHUSU

Unknown
View my complete profile

PATA HABARI KWA EMAIL

Name

Email *

Message *

CHAGUA LUGHA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

  • DADA AJUTIA KILICHO MKUTA
    MWANAMKE mmoja ajulikanae kwa jina la flora mkazi wa temeke jijini Dar es salam ,amekutwa na ugonnjwa ambao haujajulikana kwa hat\ralka mpak...

HABARI ZOTE

WADAU WANGU

chengula news. Simple theme. Powered by Blogger.