Wednesday 13 May 2015

PICHA ZA MATUKIO YANAYO ENDELEA BURUNDI


rai
Hivi karibuni Burundi imeingia kwenye headlines kutokana na machafuko ya kisiasa yanayoendelea nchini humo kufuatia Rais aliyeko madarakani Pierre Nkurunziza kutangaza kuwania nafasi ya Urais kwa awamu ya tatu .
Leo Stori mpya kutoka Burundi ni Jeshi la nchi hiyo kuamua kumpindua Rais huyo madarakani ili kuondokana na machafuko ambayo tayari yameua baadhi ya watu huku wengine wakikimbilia katika nchi za jirani.
NKUU
Meja Generali mstaafu wa jeshi la Burundi Godefroid Niyombareh na kamati yake walifikia maamuzi hayo kwa madai amekosa vigezo baada ya kuonekana kukataliwa na kukiuka katiba ya nchi hiyo
Mapinduzi ya kumtoa Rais huyo yamefanyika leo wakati akiwa Tanzania akijumuika na viongozi wengine wa Afrika Mashariki akiwemo Museni na Kagame kutafuta suluhu ya mgogoro unaoendelea nchini humo.
raia
Wananchi wakishangilia jijini Bujumbura baada ya mapinduzi hayo
Wananchi mbalimbali nchini humo walionekana kupokea taarifa hiyo kwa furaha kubwa na kupita sehemu mbalimbali huku wakishangilia.

No comments:

Post a Comment