Tuesday 28 July 2015

AMISI KIIZA ARUDISHA FADHILA SIMBA SC,SOMA HAPA

Na Paul  Chengula
 
Dar es salaam
 
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uganda, Hamisi Friday Kiiza ‘Diego’ jaja amefunga bao lake la kwanza akiichezea kwa mara ya kwanza klabu yake mpya, Simba SC katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Kombaini ya Zanzibar.
Katika mchezo huo wa kirafiki uliofanyika Uwanja wa Amaan, Zanzibar Simba SC ikicheza kwa mara ya kwanza chini ya kocha wake mpya, Muingereza Dylan Kerr iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Bao lingine la Simba SC lilifungwa na Nahodha mpya wa klabu hiyo, Mussa Hassan Mgosi.

No comments:

Post a Comment