Saturday 25 July 2015

YANGA SPORTS CLUB,YAVUNA MAMILIONI KUTOKA KWA BLACK ACES,SOUTH

        NaPaul  Chengula


MSHAMBULIAJI Mliberia wa Yanga SC, Kpah Sean Sherman (pichani) anatarajiwa kuondoka Dar es Salaam Jumatatu kwenda Johannesburg, Afrika Kusini kufanya vipimo vya afya kwa ajili ya kujiunga na klabu ya Mpumalanga Black Aces ya Ligi Kuu ya nchi hiyo.
Sherman aliyejiunga na Yanga SC Desemba mwaka jana, amepata nafasi ya kujiunga na timu hiyo na klabu yake imeridhia aende, baada ya kuleta mshambuliaji mpya, Donald Ngoma kutoka Zimbabwe. 
Sherman aliyetokea klabu ya Ligi Kuu ya Cyprus Kaskazini, Cetinkaya FC, ambayo alikuwa anaichezea kwa mkopo kutoka Aries FC ya kwao Liberia hadi sasa ameichezea Yanga SC mechi 27 na kuifungia mabao sita tu

No comments:

Post a Comment