Na KMKM itahitaji ushindi ili pia kujihakikishia kwenda Robo Fainali ya michuano hiyo kutoka Kundi A.
Timu tatu kati ya tano za kundi hilo zitakwenda Robo Fainali kuungana na washindi wawili wa kila kundi B na C pamoja na mshindi wa tatu bora kutoka makundi hayo.
KMKM na Yanga SC kila moja ina pointi tatu baada ya kila timu kushinda mechi moja hadi sasa, dhidi ya wapinzani wale wale, Telecom ya Djibouti.
KMKM imekwishapoteza mechi mbili baada ya kufungwa 2-1 na Khartoum N na 3-1 na Gor Mahia, wakati Yanga SC imepoteza mechi moja tu dhidi ya Gor.
Kocha Ally Bushiri wa KMKM alisema jana bada ya kipigo cha Khartoum kwamba watarudi Uwanja wa Taifa, Ijumaa kupigania ushindi ili kuangalia uwezekano wa kwenda Robo Fainali.
Yanga SC ina mechi nyingine ngumu dhidi ya vinara wa kundi hilo, Khartoum N ya Sudan ambayo itakuwa ya mwisho baada ya kucheza na KMKM kesho.
Yanga SC inashika nafasi ya tatu kwa pointi zake tatu, mabao manne ya kufunga na mawili ya kufungwa, wakati KMKM ina pointi tatu, mabao matatu ya kufunga na matano ya kufungwa.
Telecom ya Djibouti ambayo itacheza mechi ya mwisho na Gor Mahia kabla ya kuelekea Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam kupanda ndege ya kurejea Djibouti haijashinda mchezo hata mmoja hadi sasa baada ya kufungwa mechi zote tatu.
Ilifungwa 1-0 na KMKM, ikafungwa 5-0 na Khartoum na jana imefungwa 3-0 na Yanga SC.
Hadi sasa unaweza kusema Khartoum na Gor Mahia tayari zipo Robo Fainali, lakini nafasi ya tatu inagombewa na Yanga SC na KMKM-maana yake mechi ya kesho ni ya ‘kukata na shoka’.
No comments:
Post a Comment