Monday 3 August 2015

TAZAMA GARI LINALO PEDWA ZAIDI NA WANASOKA,MTANZANIA MMOJA NAE YUPO


Mchezo wa mpira wa miguu ni miongoni mwa kazi zenye mishahara mikubwa sana, kama ambavyo mtu kipato chake kinavyoongezeka ndivyo anavyotamani kumiliki kitu kizuri zaidi… Mastaa wa soka ni watu ambao wamekuwa na utamaduni wa kumiliki magari mengi na ya gharama ila kila mtu anapenda gari kulingana na hitaji lake au mapenzi yake
August 3 nakusogezea gari ambalo linamilikiwa na mastaa wengi zaidi wa soka.
Range_Rover_Sport_SDV6_SE_(Facelift)_–_Heckansicht,_5._September_2012,_Wuppertal
Mastaa wenye urefu kama Peter Crouch hupenda kutembelea Range Rover kwani magari ya chini huwa sio rafiki na maumbo yao. Range Rover ni gari ambalo lina thamani ya zaidi ya dola 60,000/= ambazo ni zaidi ya Tsh 120,000,000/=.
1. Peter Crouch ni staa ambae amewahi kuichezea timu ya Liverpool na sasa yupo katika klabu ya Stoke City.
article-2218994-158BF30B000005DC-348_634x730
Crouch akiingia kwenye mchuma wake wa nguvu !!
2. Robin van Persie wengi tulianza kumjua kupitia vilabu vya Arsenal, Manchester United ila kwa sasa yupo katika klabu ya Fenerbahce ya Uturuki.. Jamaa nae ana huu mchuma pia aisee !!
PAY-Van-Persie-pulled-over-by-Police
Robin Van Persie anaenda kuingia kwenye Range yake.. Hii picha ilinaswa ni kama jamaa aliingia kwenye utata na Police hivi..
  1. Dareen Bent huyu ni mkali mwingine ambae amewahi kutamba katika vilabu vya Aston Villa, Tottenham Hotspur sasa yupo katika klabu ya Derby County.
Darren-Bent-pictured-in-2011-beside-the-luxury-Range-Rover-stolen-from-his-home-at-the-weekend
Dareen Bent nae ana hii Range Rover Sport yake kali kabisa.
4. Ryan Giggs ni mkali ambae ana heshima kubwa Manchester United kabla na hata baada ya kustaafu soka, mcheki anavyoisukuma sasa Range Rover yake mtaani… taratiibu namna hii.
article-2438591-1865BD5500000578-380_634x430
5. John Terry ni nahodha wa klabu ya Chelsea lakini pia anaichezea timu ya taifa ya Uingereza.
article-2438591-1865BC8F00000578-263_634x393
John Terry yuko zake mtaani anakula stori na watu wake.
  1. Wayne Rooney nahodha wa Manchester United nae yumo katika orodha ya mastaa wanaomiliki Range Rover
1365503034
  1. Michael Essien mkali wa soka kutokea Ghana ameingia pia katika hii orodha
Michael Essien Foundation new

maxresdefault
  1. David Beckham hadi anastaafu soka alikuwa anatajwa kuwa mwanasoka tajiri Duniani, akaona sio mbaya na yeye kumiliki Range Rover yake kali kabisa!!
tyres-for-footballers-David-Beckhams-Range-Rover
Beckham na watoto wake.
9. Javier Hernandez Chicharito ni mkali wa mipira ya kuvizia jina lake lilikuwa kubwa zaidi baada ya kujiunga na Manchester United mwaka 2010.
range-rover-sport
  1. Mbwana Ally Samatta huyu ni mchezaji pekee wa Kitanzania ambae ameingia katika hii orodha, amewahi kutamba na klabu ya Simba kabla ya kutimkia TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Mbwana Samatta
Mbwana Samatta mbele ya gari yake

No comments:

Post a Comment