Saturday 1 August 2015

ZITTO KABWE AFUNGUKA HII LEO JUU YA UKAWA

ZZKKumekuwa na taarifa nyingi mfululizo kuhusu kinachoendelea CHADEMA baada ya kupokelewa kwa Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli, Edward Ngoyai Lowassa… swali ambalo ripota wa CHENGULA NEWS alimuuliza Mbunge Tundu Lissu kuhusu ishu ya mpasuko ambayo iliandikwa sana Magazetini, jibu lake lilikuwa hili  >>>> “Haya maneno ni ya siku nyingi sana na tumetabiriwa maafa tangu siku ya kwanza… Lowassa hakukaribishwa na Mwenyekiti wa CHADEMA pekeyake, Wenyeviti wa UKAWA wote walikuwepo kwenye stage. Anaesema UKAWA imeteteleka hayo maneno hayataisha” — Tundu Lissu.
Magazeti yameendelea kuandika kuhusu stori ya kinachoendelea CHADEMA, gazeti la Raia Tanzania August 01 2015 limebeba headline hii >>> “Dk. Slaa ajivua uanachama, ni siku chache baada ya kujiuzulu Ukatibu Mkuu, arejesha nyaraka, gari” >>>
Zitto Kabwe amepost picha ya gazeti hilo @Instagram na kuyaandika haya >>> Siasa zinabadilika sana. Siamini kama hili laweza kutokea, lakini wiki kwenye siasa ni kubwa mno. Sisi wengine tunatazama tu maana tulipita kwenye changamoto hizi“– @

No comments:

Post a Comment