Awali, mchezo huo ilikuwa ufanyike Jumapili, lakini Ofisa Habari wa Simba SC, Hajji Sunday Manara amesema kwamba umeahirishwa kupisha uzinduzi wa kampeni za vyama vya siasa kuelekea uchaguzi Mkuu.
Mchezo huo unatarajiwa kuwapa fursa wapenzi wa Simba SC kumuona kwa mara nyingine mshambuliaji wao mpya, Kelvin Ndayisenga aliyesajiliwa kutoka Burundi.
Kubwa zaidi- mchezo huo utazidi kumpa picha halisi ya maendeleo ya kikosi chake, kocha mpya Muingereza Dylan Kerr ambaye hadi sasa ameiongoza timu hiyo kushinda mechi zote nane za kirafiki.
Simba SC ya Kerr imezifunga 2-1 Zanzibar Kombaini, 4-0 Black Sailor, 2-0 Polisi, 3-0 Jang’ombe Boys, 3-2 KMKM zote Zanzibar na 1-0 SC Villa na 2-1 URA zote za Uganda Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment