Ni July 15, 2016 ambapo Malkia wa uswazi, Sara Kaisi aka Shaa amefunguka kupitia chengula news na kuelezea sababu za kuondoka kwenye uongozi wake wa zamani.
Akizungumza na chengula news staa huyo alisema…’Nimekuwa
na ndoto ya muda mrefu kama ya miaka mitano iliyopita tumeona wasanii
ambao niliokuwa nao MJ Records wakina Izzo Bizness amesimama mwenyewe
ukija kwa Quick Rocka nae kafungua studio kwahiyo huu ni muda wangu’– Shaa
‘Maamuzi ya mimi kwenda kwenye
uongozi wakina Tale ilikuwa baada ya mimi mkataba wangu kumalizika
kwenye lebo ya Unity Entertainment ya AY nilifanya nao kazi nzuri mpaka
zingine zikakubalika ila maamuzi yangu kwa 2016 kazi zangu zitasimamiwa
chini ya record label yangu’- Shaa
No comments:
Post a Comment